Hot!

KWA NINI BIASHARA NYINGI ZINASHINDWA KUENDELEA?Ni kukosa Ubunifu Au Uzembe?


 Wakati Fulani nilihudhuria mafunzo ya ujasiriamali yapata miaka 10 iliyopita. Mtoa mada alitaka kujua endapo kila mshiriki angepewa milioni mia moja angefanya nini. Katika majibu yaliyonishngaza ni pale mshiriki mmoja aliposema yeye angejenga hoteli eti kwa sababu tuu baba mkwe wake alimwambia kuwa hoteli zinalipa.

Haikunishangaza mtoa mada alipotaka kujua sababu ya kijana Yule kumwamini baba mkwe wake kiasi kile. Maya zaidi ni pale alipoulizwa kama baba mkwe wake ana hoteli au aliwahi kumiliki hoteli, kijana huyo alisema hapana.

Ni kawaida ya wajasiriamali wengi kufanya vitu kwa sababu tuu wengine wanafanya bila kujali namna ya kufanya kitofauti ili kuvutia wateja zaidi. Katika shughuli zangu za ushauri wa biashara nimewahi kukutana na mama mmoja aliyekuwa anatubu na kujuta baada ya kushindwa kurudisha mkopo aliochukua ili kuboresha biashara yake ya kupika na kuuza vyakula almaanufu mama lishe/ntilie, alisema

“…….tulianza kama wamama  watatu hivi. Hakika wateja walikuwa wengi na tulidhani kuna haja ya kuongeza mtaji ndipo nikakopa. Katika kipindi cha miezi sita tuu tayari kulishakuwa na wakina mama wengine zaidi ya kumi waliojiunga na kuanza kufanya biashara ya kuuza chakula. Kiukweli ilikuwa ni kama tumewafumbua macho na kuwaonesha fursa ambayo walikuwa hawajaifahamu bado. Cha kushangaza nikwamba kati yetu wote hakuna aliyekuwa akitoa huduma ya tofauti na wenzake. Yani ni wali nyama ule ule na bakuli ya maharage/mchicha pembeni. Taratibu tukaanza kuwekeana vinyongo kwa ajili ya kugombania wateja. Sasa hivi ninavizungumza na wewe mama (jina limehifadhiwa) anamtuhumu mama (jina limehifadhiwa) kwa kumloga ili biashara yake isifanikiwe…”

Hii ni sehemu ndogo tuu ya mifano ninayokutana nayo kila siku ninapozungumza na wajasiriamali. Yamkini wajasiriamali tungefahamu ni kwa namna gani ubunifu na huduma bora kwa wateja unavoweza kuleta tija na ufanisi katika biashara. Tunapaswa kuamka na kuachana na fikra za kizamani katika uanzishwaji na uendeshaji wa biashara zetu.

Nani kasema kuwa eti kwa sababu baba mkwe au mtu Fulani kasema bishara ya hoteli inalipa basi uanzishe biashara ya hoteli. Je unajua wateja wa hoteli wanataka nini? Je unajua kuna kundi gani la wateja wa hoteli waliosahaulika na mfumo wa hoteli zilizopo. Labda wapo ambao shida yao ni kulala tuu – nani kakwambia lazima uwawekee self contained yako na mi breakfast yako inayofanya gharama kuwa maradufu?

Pengine wapo wanaotaka kuja kipumzika na familia nzima – nani kakwambia uwajengee jihoteli lako lenyevyumba vilivyopangana kama vya mabweni ya vyuo vikuu? Amka fikiria, kuwa mbunifu fursa bado zipo achana na mawazo ya kizamani ya kuiga kila kitu?

Kwa wale walio mazingira kama ya Yule mama lishe aliyenitembelea ofisini kwangu: Nani kakwambia kila mtu anapenda miwali yenu ya nyama na maharage mliyokaanga kwa maguta yenye cholesterol isiyo na kipimo? Nani kawaambia kila mtu anapenda kuja na kula anachokikuta?

Yawezekana wapo wanaopenda vyakula vya asili vilivyochemshwa bila mafuta ( wazungu wanaviita natural foods). Kunaweza kukawa pia na wale ambao wanaopenda kupikiwa kwa mahitaji maalumu. Amkeni kuweni wabunifu, wateja hawaletwi kwa kulogana.

Mama lishe niliyemshauri leo ananishukuru sana. Tunavozungumza yeye kaachana na miwali yenu ya mafuta na kukaanga. Hivi sasa anauza ugali wa mtama, ndizi mchemsho, udaga samaki wa kuchemsha..nk. Hata wenzake wamejaribu kumuiga lakini wameshindwa. Kwa kifupi amegundua kukaa kwake kijijini kumsaidia kujua kupika vyakula vya kiasili kwa ladha ya kipekee isiyowezwa kuigwa na mtu yoyote.

Yule kijana alifanikiwa kupata mkopo ingawa sikumbuki ni shilingi ngapi. Ninachojua ni kwamba hoteli yake ipo katika orodha ya hoteli zinazotarajiwa kupigwa mnada. Namwombea mugu ajitabue na kubadilika. Maana mpaka sasa nahisi hajaelewa somo. Yeye anachojua ni kuilamu tuu serekaliu eti imesababisha biashara yake kuwa ngumu. Mh! kwa kweli safari yake bado ndefu.

Hapo ni kuhusu ubunifu tuu kwa leo sitaki hata kuzungumzia makosa tunyofanya katika kuwahudumia wateja. Siku nyingine nitakuja na rafiki yangu Dotto Bulendu anisaidie kuwaeleza wakati tulipokuwa safarini akamuuliza muhudumu wa ndege kama kuna kahawa au tangawizi alijibiwa nini…

Nawatakia siku njema.

0 comments:

Post a Comment