Mwaka 2009 Ben Mezrich aliandika kitabu kilichoitwa, “Accidental Billionnaires: The
founding of facebook, a tale of sex, money, genious and betrayal”. Kwa hakika kitabu hiki kinatoa
fundisho kubwa sana kwa wajasiriamali wa kitanzania na duniani kwa ujumla.
Ukisoma kitabu hiki kilichosheheni utafiti
yakinifu wa habari ya kuundwa kwa facebook – mtandao maarufu wa
kijamii, utagundua umuhimu wa ubunifu na jinsi ya kuhakikisa kuwa ubunifu huo
unalindwa na kuwa endelevu.
Pamoja na kwamba wazo la kuanzisha facebook
lilianzia kwa mapacha wawili (maarufu kwa jina la Winklevos twins) na kuchagizwa na mtaji wa kwanza (capital seed)
uliotolewa na Eduardo Saverin (rafiki aliyekuwa anaishi na mmiliki wa sasa wa
facebook), ni Mark Zuckerberg pekee anaeonekana shujaa kwa sasa.
Ndio ubunifu ni mzuri lakini tunapaswa kuwa
makini na tunaowashirikisha mawazo yanayotokana na ubunifu wetu. Mark Zukerberg
alikuwa na utaalamu wa kuweza kuanzisha facebook lakini je asingekutana na hao
mapacha angeweza kuwa na hilo wazo?
Katka moja ya majadiliano kati ya Zuckerberg
na Winklevos twins, kunaibuka hoja ya facebook itakuwa na utofauti gani na
mitandao mingine za kijamii (kwa wakati huo twiter na My Space). Kwa the
winklevos twins jibu lilikuwa ni rahisi tu – hwrvard.edu. Waliamini kuwa na mtandao wa kijamii wenye domain ya Harvard
kungewavutia wanachuo wengi kujiunga.
Tunkumbuke kuwa nilipowasimulia hadithi ya
mama lishe tuliona umuhimu wa kuwa na kitu tofauti kwenye biashara. Kwa facebook
ilikuwa hivyo hivyo. Mbali na kuwa na domain ya havard, kadiri siku zilivokuwa
zinaenda Mark Zuckerberg na timu yake waliendeleza ubunifu na kuifanya facebook
kuwa chaguo la wengi katika jamii. Taratibu thamani ya facebook ikapanda mpaka
kufikia hatua ya Mark Zukerberg kuwa tajiri kijana zaidi duniani.
Mbali na
kuwa mbunifu changamoto kubwa huja katika kuhakikisha ubunifu unalindwa na kuwa
endelevu. Taaluma ya biashara inaonesha kuwa zipo njia mbalimbali mbali za
kutunza ubunifu. Njia hizo zinatofautiana kuendana na mazingira, malengo na
wakati mwingine aina ya biashara.
Kwa mfano kama biashara inahusu uzalishaji wa
chakula au kinywaji njia rahisi ni kujimilikisha kanuni (formular) kwa
kuisajili kisheria na kuhakikisha haiigiki kirahisi – Coca Cola, watengenezaji
wa pipi za ivory na kampuni zinazotoa huduma ya teknolojia wamefanikiwa sana
kwa kutumia njia hii.
Endapo biashara inahusu kutoa huduma utunzaji
wa ubunifu unaweza kuwa changamoto kwa kiasi fulani. Na wakati mwingine
wajasiriamali/wamiliki wa biashara wanalazimika kuchanganya ubunifu na unafuu
wa gharama. Biashara zinazofanikiwa kwenye Nyanja za usafiri, hoteli na utalii
zimekuwa zikitumia sana kwa kutumia mbinu hii.
Wakati mwingine inapokuwa vigumu kushindana
kwenye ubunifu au mchanganyiko wa uubunifu na upungufu wa bei, njia pekee
inayobaki ni kumnunua mpinzani wako au mpinzani wa mpinzani wako. Mara nyingi
matokeo ya njia hii ni kujimilikisha soko kwa kubaki mwenyewe sokoni au
kupunguza idadi ya washindani ili kuongeza ufanisi.
Mfano mzuri ni tukio la miaka ya hivi
karibuni la facebook kuinunua kampuni ya watsap ili kupunguza usindani. Yote kwa
kwa yote habari ya facebook inatupa fundisho la historia nzima ya jinsi
mjasiriamali wa kawaida anavyoanza na ubunifu wake na changamoto anazoweza
kuzipitia kabla ya kupata mafanikio.
Kwa Winklevos twins tunapata fundisho la kuwa
makini na ubunifu wetu, kwani wapo waliozoea kutembelea nyota za watu kwa kuiba
mawazo ya watu wengine na kuyafanya ya kwao katika biashara. Laiti kama
wangeingia mkataba wa kisheria na
Zuckerberg kwa kumuajiri kama mtaamu wa kompyuta leo hii face book ingekuwa ya
kwao.
Kwa Zuckerberg tunapata fundisho la
kuhakikisha ubunifu ni endelevu. Kwa kuinunua watsap facebook itabaki kuwa moja
ya mitandao bora ya kijamii kwa muda mrefu. Ewe mbunifu mwenzangu umeshafikiria
namna ya kutunza ubunifu wako? Au unangoja mpaka uanguke kama mimi halafu ubaki
kuilamu serekali yako?
Mimi nilianguka nikaamka. Naamini sitaanguka
tena maana nimejifunza mengi kwenye kuanguka kwangu. Winklevos twins na Eduardo
Saverin waliangushwa na Zuckerberg. Sina uhakika kama walishaamka au la? Ila nina
uhakika anguko lao ni fundisho kwa wengi.
Amka mjasiriamali mwenzangu kuwa mbunifu. Hata
mdogo wangu Humphrey Mgonja kaamua kuwekeza kwenye ubunifu katika tasnia ya
uandishi wa habari; na ndio maana kaiona fursa kwenye kanisa la viziwi na
habari ya mbuzi wanaoishi mjini kama binadamu. Fursa ambazo waandishi wenzake
hawakuziona hapo mwanzo
Kwa heri kwa leo ila nakusisitiza tena ndugu
yangu uamke ili miaka ya mbeleni Ben Mezrich apate kuandika kitabu juu jinsi
ulivoamka kutoka kwenye anguko lako na kuwa mfanya biashara uliyefanikiwa zaidi
Tanzania.
0 comments:
Post a Comment