Takribani miongo mitatu iliyopita muokota
makopo alikuwa akionekana mwehu. Yani kulikuwa na msemo maarufu uliosema “ unaniita kichaa kwani naokota makopo”
kwa wakati huo ilikuwa ni nadra kumkuta binadamu mwenye akili timamu akiokota
makopo mitaani.
Ama kweli siku hazigandi. Nimelazimika
kuamini dunia inabadilika. Ndio! Tanzania inabadilika na tunaweza kusema
Daresalam inabadilika na itaendelea kubadilika. Eti leo muokota makopo anaitwa
mjasiriamali.
Nimeshtushwa na kasi ya waokota makopo ambao
kwa hali inavyoenda inaweza kufika mahali wakawa kero kwenye nyumba za watu. Imekuwa kawaida kwa siku za
hivi karibuni kusikia mtu akigonga geti. Eti anauliza kama kuna chupa za
plastiki.
Ni hali hii inayonivutia na kunifanya niwaze
kufanya utafiti juu ya biashara hii ya kuokota makopo. Naanza kujiuliza nini
kimeongezeka kwenye chupa hizi za plastiki ambacho hakikuwepo miongo miwili
iliyopita? Najiuliza tena ni nini kilichoongezeka katika makopo na vyuma chakavu
vya sasa ambacho hakikuwepo miongo miwili iliyopita?
Katika kutafiti kwangu nagundua kuwa hakuna
kilichobadilika katika chupa makopo au vyuma chakavu. Vyuma ni vile v ya miongo
miwili iliyopita. Hali hii inanivutia kutaka kujua kutoka kwa anaefanya biashara
ya kuuza vyupa vya plastiki au vyuma chakavu. Kwakuwa muda umeshaenda najipa
moyo kwamba kesho lazima nitafute mtu
anaefanya niashara hii ili ipate undani.Kama ilivyo ada kwa wengi naamua kwenda kuimalizia siku yangu katika ukumbi wa mazoezi ya viungo. Najisogeza kivivu huku nikitamani muda uende haraka – asikudanganye mtu , hakuna kazi ngumu kama kufanya mazoezi ya viungo.
Ninachokikuta kwenye ukumbi wa mazoezi
kinarudisha fikra zaku masaa kadhaa nyuma.
Namuona kijana mmoja aliye makini sana. Mkononi kashika mfuko wa
plastiki almaarufu mifuko ya Rambo. Ukimtazama kijana huyu anavoangalia watu
kwa makini utadhani ni mlinzi wa ukumbi au askari magereza anaesimania wafungwa
wakifanya kazi ngumu.
Umakini wote wa kijana huyu umelenga kwenye
kuhakikisha anamuwahi kila anaekunywa maji ili amuachie chupa tupu baada ya
kumaliza. Dah! Kumbe utafiti niliopanga kuufanya kesho ninaweza kuufanya leo.
Namdadisi kijana huyu muokota chupa za maji
ili kujua kwa nini ameamua kufanya kazi iyo. “…..hii kazi inalipa sana braza. Kwa siku sikosi elfu 5 mpaka kumi. Kimsingi
nimeamua kujiajiri na ninajivunia kwa kazi ninayofanya……” ananiambia.
Kumbe janga la uchafuzi wa mazingira lmegeuka
kuwa fursa. Mwalimu wangu wa ujasiriamali aliwahi kuniambia kuwa, biashara nyingi zilizofanikiwa ni zile
zilizotokana na changamoto.
Hapo ndipo ninapokumbuka safari yangu ya nchi
moja ya jirani pale niliposhudia kampuni inayokusanya kinyesi cha binadamu na
kukigeuza kuwa mbolea na baadae kuwauzia watu. Nakumbushwa zaidi na habari ya
kampuni ya kigana inauotumia taka ngumu kutengeneza mbolea asilia.
Hakika namaliza siku nikiwa nimehamasika. Najiapa
moyo, najiambia kuwa ipo siku na mimi nitabadilisha changamoto kuwa fursa. Amka
mjasiriamali mwenzangu. Amka tufikirie nje ya boksi ili tuvumbue ni changamoto
gani tunazoweza kuzigeuza kuwa fursa.
Kwaheri kwa leo mjasiriamali mwenzangu ila
nakuomba unapowaza juu ya kugeuza changamoto kuwa fursa ujiulize: yupo wapi Yule
mtanzania aliyevuma kwenye vyombo vya habari kwa kutengeneza roboti kwa ajili
ya kulinda usiku? Yupo wapi yule kijana aliyegundua teknolojia ya kuzima umeme
kwa kutumia simu hata kama mtumiaji yupo kilomita elfu moja kutoka ilipo nyumba
yake?
Sikutishii ndugu yangu, nakupa tuu changamoto
ili uweze kufikiri nje ya boksi. Haya basi pumzika. Ingawa wakati unapumzika
nakuasa ujiulize ni kwa nini mgunduzi wa power bank ya Puku (ambaye ni
mtanzania) kaisajili kampuni yake
marekani badala ya Tanzania?
0 comments:
Post a Comment